Jumamosi 28 Juni 2025 - 09:19
Imam Hussein (as) ni kielelezo cha uhuru na haki; maombolezo ni haki ya raia na urithi wa muqawama

Hawza/ Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Sajid Ali Naqvi, katika ujumbe wake kutokana na mnasaba wa kuwadia kwa mwezi mtukufu wa Muharram al-Haram, amesisitiza kuwa uendeshaji wa maombolezo kwa ajili ya Imam Hussein (as) ni miongoni mwa haki za wazi, za kisheria na za kidini za raia wote, na amesisitiza juu ya umuhimu wa kulinda heshima ya siku za maombolezo, kuimarisha umoja wa Kiislamu na kupambana na harakati zinazoeneza migawanyiko.

Kwa mujibu wa ripoti ya kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Sajid Ali Naqvi, Raisi wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan, katika ujumbe wake kutokana na mnasaba wa kuingia mwezi wa Muharram al-Haram, amesisitiza kuwa kuandaliwa kwa vikao vya maombolezo ya Imam Hussein (as) ni haki halali, ya kisheria na ya kidini ya kila mwananchi, na kwamba ni wajibu kulinda heshima ya siku hizi tukufu, kuimarisha mshikamano wa Kiislamu, na kukabiliana na harakati zinazoleta fitina na kusambaratisha umoja.

Katika ujumbe huo, huku akiashiria wajibu wa pamoja wa maulamaa wa madhehebu mbalimbali, waimbaji wa nauha, na jamii kwa ujumla, amesema: Wote wanapaswa kwa kuheshimiana, kuchangia kuimarisha mazingira ya undugu, mshikamano wa Kiislamu na maisha ya pamoja yenye amani.

Mwanazuoni huyu mashuhuri wa Kipakistani ameeleza bayana kuwa: Mwezi wa Muharram si tu ukumbusho wa tukio lenye uchungu la Karbala, bali ni fursa ya kutafakari juu ya malengo, dira na ujumbe wa harakati ya Imam Hussein (as). Vikao vya maombolezo ni njia ya kuhuisha mwenendo wa Kihusseini na kufafanua sura halisi ya wapinga dhulma mbele ya watawala madhalimu wa kila zama.

Ni lazima kutumia fursa hii ya kiroho kwa kurejea masomo ya Ashura na kuchora njia za vitendo za kukabiliana na changamoto za zama zetu.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha